CONSTITUTIONA WRITING

Wednesday, January 1, 2014

WATU HATARI

                  Kuna watu wa ajabu wenye mambo ya kushangaza katika dunia hii. Kutokana na imani yangu Mungu tunaye mmoja na ndiye anayestaili kuabudiwa. Lakini wanadamu baadhi wamejifanya kuwa miungu watu  kutokana na sababu kubwa mbili. Sababu ya kwanza msingi wake unatokana na kuwa na mamlaka juu ya  watu wengine. Mamlaka yamewanya baadhi ya watu wawadharau wengine hadi  kuwadhalilisha utu wao. Sababu ya pili ni kuwa na umiliki wa mali (rasilimali pesa). Kuna baadhi ya watu wanataka kuabudiwa na kujiona kwamba kila wanachosema ni sahihi kuliko wengine. Sababu nyingine ambayo kwa sasa haina nguvu sana ni elimu. Kwamaana unaweza ukawa na elimu lakini kama hauna mamlaka ya kiutawala au pesa au kuwa karibu na watawala unaweza usiwe na nguvu katika dunia ya sasa. Lakini pamoja na hayo kuna watu wanotumia mwanya wa ujinga wa watu kuwatawa kifikra hali ambayo utengeneza umungu MTU.
            Hali hii yakutaka kuabudiwa imekuwa ndiyo chanzo cha migogoro mbalimbali inayoendelea hapa duniani. Ukichambua kwa kina  utaona  hawa watu wanaojiona bora zaidi ya wengine ni wale ambao hofu ya Mungu haipo ndani ya mioyo yao. Makundi haya yamwshika   hatamu si kwenye siasa bali hata kwenye majumba ya ibada kama makanisa na misikiti. Ndiyo wanaopewa kipaumbele kwa mambo mengi.

      Pia watu wanojiona bora zaidi ya wenzao huwa na sifa ya ubinafssi. Ukimkuta ofisini mali ya umma anaitumia kama vile ni mali yake. Mtu wa  sampuli hii ni mwepesi kuchukua hatua kali kwa waliochini yake pindi wanapokosea huku akisahau maovu ambayo anayafanya yeye    mwenyewe.  Akiachishwa cheo huwa siyo wepesi wakuonyesha ushirikiano bali huwa na majungu na ni hatari kwani wanaweza kufanya mbinu zozote zile mbaya amabzo zinaweza kumhatarisha mtu mwingine aliyepewa hiyo nafasi.
     Mara nyingi hawa watu wakujikweza na kupenda kuabudiwa, huwa ni wanafiki ikiwa na maana kwamba hupenda kuonekana wasafi mbele za watu kwa gharama zozote iwe kwa kutumia cheo au pesa ili mradi jamii iwaone wanafaa. Watu hawa, vigumu kuleta mabadiliko kani  wao wenyewe hawajabadilika (not transformed therefore it is difficult to transform others).
     Kutokana na tabia za watu hawa husababisha migogoro kujitokeza kati yao na jamii. Kwa mfano mwenye mamlaka akiwadharau waliochini yake hawatamheshimu na matokeo yake kama ni wafanya kazi utafuta sababu na mbinu za kumwonyesha kwamba hawamkubali. Kwa kufanya hivyo migogoro upamba moto.
    Kwa mwenye pesa utaka kumiliki kila nyenzo muhimu katika maisha ikiwa ni pamoja kupanga bei sokoni na kudhulumu rasilimali za wanyonge. Na wanyonge wakijitambua wakaona wanafanyiwa ndivyo sivyo upambana kwa migomo na maandamano kwa maana sheria mara nyingi huwa upande wa mwenye pesa na hata akiwa na kosa mamlaka zinazohusika umwajibisha kifallme suala amabalo huchochea migogoro kwa wananchi.
         Ukikosa hofu ya Mungu kama binadamu inapelekea mtu kutokuwa na hekima na busara matokeo yake ni kutoa maamuzi kwa misingi yakutaka kujiona bora zaidi na kudharau wengine kwa misingi ya fedha, elimu na nafasi/ mamlaka aliyonayo mtu. Pia hali hii huchochea kutotendeka kwa haki na ibinadamu hatimaye migogoro. Wanadamu wamekengeuka mpaka kufikia hatua ya kuwajeruhi watu wengine kimwili na kiroho ambao harakati zao zinapingaukiukwaji wa haki za binadamu na unyonyaji.

No comments :

Post a Comment