CONSTITUTIONA WRITING

Sunday, September 29, 2013

TRUE LOVE

          Mapenzi ya kweli kwa unayempenda ni nguzo muhimu katika kujenga taifa la watoto wasio wa mitaani. Kama watu mnapendana ni vigumu kuachana. Kikubwa zaidi kama una mpenzi wako jitahidi kuwa muwazi kwake ili ajenge imani na wewe. Jadili pamoja panapotokea jambo la kutatiza. Pia kuwa makini siri au madhaifu ya mpenzi wako usimwambie mtu yeyote maana akifahamu atapoteza imani na wewe. Kuna wengine midomo haina breki hasa vijana wenzagu. Kitendo cha kumwaga siri za ndani unatengeneza mwanya wa wengine kuingilia penzi lenu.
         Achana na tamaa, rizika kwa kile unachokipata. Siku hizi watu wanatamaa akiona rafiki yake mpenzi kamnunulia kitu kizuri basi huanza fujo kwa mpenzi wake na kumdharau eti kwa kuwa hajafanyiwa kama rafiki yake- huo ni ulimbukani kwani anyepanga riziki ni Mungu.  Kama  shida ni gari kaa na mpenzi wako ili mpange mkakati wa kuwawezesha kupata hicho unachokihitaji. Mkipanga pamoja na mkafanikiwa kukipata  ukiwa na mwenzi wako faida zake ni nyingin kwanza ni heshima katika jamii, pili mpenzi wako atakuthamini sana na kuona wewe wa maana sana katika maisha.
       Acha kuwasifia wapenzi wa watu wengine mbele ya mpenzi wako. halii hii yakusifia wapenzi wa wengine inamfanya mpenzi wako akuone kama bendera fuata upepo hivyo unaweza kumjengea mazingira mpenzi   wako asiwe na imani na wewe.
      Tumia maneno ya upole pale kuna potokea kukwaruzana na katika kutafuta mwafaka msiwe kama mechi ya kutafuta mshindi bali jishushe tabasamu kidogo, mshike ata shavu mwenzio ili kujengana kiaiokolojia. Kuna wengine mbinu hizi hawazitumii ndio maana wanaweza kununiana hadi mwaka na hatimaye kuachana. Na kama wamezaa pamoja basi watoto huumia kwani hupelekea wakose malezi ya upande mmoja. Kila siku kuwa na hali kama ile ile ya mwanzo wa mahusiano wakati mnatongozana. Nina amini mkifanya hivyo migogoro ya ndoa na kutelekezwa watoto ambako kunapelekea kuongezeka kwa watoto wa mtahani na mmomonyoko wa maadili kutapungua kwa kiwango kikubwa.

No comments :

Post a Comment